Tafuta

2025.06.06 Papa akutana na Bwana  Antonio Costa, Rais wa Bunge la Ulaya. 2025.06.06 Papa akutana na Bwana Antonio Costa, Rais wa Bunge la Ulaya.  (@VATICAN MEDIA)

Papa Leo akutana na Rais wa Bunge la Ulaya

Ijumaa Juni 6 Papa Leo XIV alikutana na Rais wa Bunge la Ulaya,Bwana Costa,ambaye mara baada ya mkutano huo alikutana na Kardinali Pietro Parolin,Katibu Mkuu wa Vatican,akisindikizana na Monsinyo Mirosław Wachowski,Katibu Msaidizi kwa ajili ya Mahusiano na Mataisaha na Mashirika ya Kimataifa.Katika muendelezo wa mazungumzo muktadha wa sasa wa kimataifa ulishughulikiwa,kwa kurejea juu ya migogoro ya Ukraine na Gaza.

Vatican News

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Vyombo vya habari Vatican, Papa Leo XIV, Ijumaa tarehe 6 Juni 2025 alikutana katika Jumba la Kitume mjini Vatican, na Rais wa Bunge la Ulaya, Bwana António Costa, ambaye mara baada ya mkutano huo alikutana na Kardinali  Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican, akisindikizana na Monsinyo Mirosław Wachowski, Katibu Msaidizi wa Vatican kwa ajili ya Mahusiano na Mataisaha na Mashirika ya Kimataifa.

Papa Leo XIV akutana na Rais wa Bunge la Ulaya Bwana Costa
Papa Leo XIV akutana na Rais wa Bunge la Ulaya Bwana Costa   (@VATICAN MEDIA)

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, "katika mazungumzo yao, Srkretarieti ya Vatican walionesha uhusiano mwema kwa sehemu mbali mbali kati ya Vatican na Umoja wa Nchi za Ulaya na na shauku  ya kuzidisha mijadala kuhusu masuala yenye maslahi kwa pamoja, hasa kuhusiana na pendekezo la kuanzisha mfuko wa kimataifa wa kuondoa njaa duniani na kukuza maendeleo ya nchi maskini zaidi. Katika muendelezo wa mazungumzo hayo, muktadha wa sasa wa kimataifa ulishughulikiwa, kwa kurejea juu ya migogoro ya Ukraine na Gaza."

Baada ya mkutano na Papa,Rais wa Bunge la Ulaya alikutana na Katibu Mkuu wa Vatican
Baada ya mkutano na Papa,Rais wa Bunge la Ulaya alikutana na Katibu Mkuu wa Vatican   (@VATICAN MEDIA)
Mkutano wa Rais wa Bunge la Ulaya na Sekretarieti ya Ulaya
Mkutano wa Rais wa Bunge la Ulaya na Sekretarieti ya Ulaya   (@VATICAN MEDIA)
06 Juni 2025, 18:13